Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida
(Hospitali ya Mkoa)

GARI JIPYA LA WATUMISHI LAZINDULIWA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SINGIDA

Posted on: November 30th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Beneth Mahenge azindua rasmi gari la Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa

Singida.

Uzinduzi huo wa gari la Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida umefanyika leo tarehe 30/11/2021 katika

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida eneo la Mandewa ambapo Mkuu huyo wa Mkoa wa Singida alizindua rasmi gari la

watumishi wa Hospitali ya Rufaa mpya aina ya Coaster ambayo imenunuliwa na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida

kwa mapato ya ndani.

Akiongea katika uzinduzi huo Daktari Mahenge alisema kwamba gari hilo litawasaidia sana Watumishi wa Hospitali ya

Rufaa ya Mkoa wa Singida kuwahi kazini pia litawasaidia kwenye shughuli za misiba ambayo kisheria inapaswa

kusimamiwa na mwajiri. Aidha Daktari Mahenge aliutaka uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida kulisimamia

vizuri gari hilo na kuweka robo ya gharama zilizotumika kulinunua gari hilo kwa ajili ya matengenezo ili hata ikitokea

amekuja Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida baada ya miaka 20 alikute gari hilo likiwa zima.