Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida
(Hospitali ya Mkoa)

MWENYEKITI WA BODI YA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SINGIDA AUPONGEZA UONGOZI WA HOSPITALI

Posted on: November 30th, 2021

Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida Jaji Mstaafu Fatuma Masengi ameupongeza

uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida kwa kutoa Motisha mbalimbali za watumishi katika hospitali hiyo.

Bi Fatuma Masengi ameyasema hayo leo tarehe 30/11/2021 katika kikao cha Bodi ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa

Singida baada ya kupokea taarifa ya watumishi kwa kipindi cha kuanzia Julai 2021 hadi Novemba 2021. Kwa mujibu wa

taarifa hiyo Watumishi wote walioenda likizo kuanzia Julai 2021 mpaka Novemba 2021 wamelipwa pesa zao za likizo na

wengine wanaenda kwa kipindi hiki wanaendelea kulipwa, posho inayotokana na pesa za Bima imelipwa kwa watumishi

wote hadi watumishi wanaojitolea na waliopo mafunzo kwa vitendo wamelipwa, madeni ya likizo, postemoterm, posho ya

masaa ya ziada na posho ya kuitwa kazini ya mwaka 2018/2019 na 2019/2020 yamelipwa, watumishi 84 wamewezeshwa

na Hospitali kuhudhuria mafunzo mbalimbali, watumishi 24 wamehudhuria Makongamano mbalimbali ya kitaaluma na pia

bajeti ya posho ya kujikimu imepanda kutoka 8,500,000/= hadi 12,000,000/= na posho ya masaa ya ziada imepanda

kutoka 8,500,000/= hadi 12,000,000/=.

Mwenyekiti huyo alisema mambo yote haya ambayo wamefanyiwa Watumishi kwa kipindi hiki kifupi ikiwa ni pamoja na

kununuliwa kwa bus ya watumishi aina ya Coaster sio ya kubeza.